Jumapili 30 Agosti 2026 - 12:17
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Inaendelea kwa Misingi ya Nguvu, Uwezo na Kumtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu

Hawzah/ Ahmad al-Khatib amesema: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kwa misingi ya dhana za nguvu, uwezo na kumtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu; iwe katika kuendelea kujenga nguvu za kijeshi, uchumi wa kustahimili vikwazo, au katika siasa za kimapinduzi ambazo kwa mara nyingine zinachora ramani mpya ya ushawishi katika eneo la Asia Magharibi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza kutoka Tehran, Sheikh Ali Ahmad al-Khatib, Naibu Rais wa Baraza Kuu la Mashia wa Lebanon, katika Mkutano wa 40 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu uliofanyika Alhamisi, tarehe 5 Shahrivar (27 Agosti 2026), ukiwa na ushiriki wa wageni 80 kutoka nje katika Ukumbi wa Mikutano ya Viongozi wa Nchi, alianza hotuba yake kwa kutoa salamu za pole za dhati kwa uongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ukiongozwa na Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, kwa mnasaba wa kutimia siku 40 tangu kuuawa kishahidi kwa kiongozi mashahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei, Mwenyezi Mungu amrehemu, pamoja na kutoa salamu za pole kwa wananchi wapendwa wa Iran.

Pia, kwa mnasaba wa kuzaliwa Mtume Mkuu (s.a.w.w.), aliwapongeza wananchi Waislamu wa Iran, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Waislamu wote na washiriki wa mkutano huu kwa mnasaba huo.

Naibu Rais wa Baraza Kuu la Mashia wa Lebanon aliongeza kusema: Yeyote anayezuia kulazimishwa utawala wao juu ya rasilimali za dunia huchukuliwa kuwa adui anayestahili kuondolewa na kutupiliwa mbali; na yeyote anayeungana nao, hata katika uhalifu wao, si chochote zaidi ya chombo cha kutekeleza malengo yao, na wao hawana heshima yoyote kwa maslahi yake wala mipaka yake binafsi.

Aliendelea kusema: Kwa namna hiyo, mwenendo wa maendeleo ya kijeshi, kiteknolojia na akili bandia leo unaelekea katika kuharibu mafanikio yote ya wanadamu katika nyanja ya haki na maadili. Na mbele ya wimbi hili lisilo na mfano la ukatili, hakuna anayeweza kusimama isipokuwa Mtume Mtukufu (s.a.w.w.), ambaye leo ametukusanya kwa ajili ya kushikamana na ujumbe wake; Mtume ambaye ni muhtasari wa Utume wote, dhihirisho la maadili ya kibinadamu na fadhila za kimaadili, na mwanzilishi wa ustaarabu wa kwanza wa kina wa kibinadamu wenye nyanja za kiroho, za mbinguni na za kidunia, ukiwa na uwiano wa ubunifu.

Al-Khatib alisema: Sheria ya Mtume wa Uislamu imekuwa Sheria yenye urahisi na wepesi, ambayo pamoja na changamoto zote, ni rehema kwa walimwengu. Ndani ya Sheria hii kuna utamaduni wa Muqawama dhidi ya kila uchokozi usio wa haki na kila mradi wa kishetani usio na busara.

Akizungumzia Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, alisisitiza: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo, ikitegemea fikra za mwanafikra na mwanastratejia mkubwa katika historia ya zama za sasa, yaani kiongozi shahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei, Mwenyezi Mungu amrehemu, na ikiwa na imani thabiti katika Uislamu halisi wa Muhammad, imesimama mbele ya waasi wakubwa zaidi duniani na madola yenye uhalifu mkubwa zaidi katika historia ya mwanadamu.

Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Mashia wa Lebanon aliongeza: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kwa misingi ya dhana za nguvu, uwezo na kumtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu; iwe katika kuendelea kujenga nguvu za kijeshi, uchumi wa kustahimili vikwazo, au katika siasa za kimapinduzi ambazo kwa mara nyingine zinachora ramani mpya ya ushawishi katika eneo la Asia Magharibi.

Aliendelea kusema, akizungumzia Wiki ya Umoja wa Kiislamu: Ninatumia fursa hii yenye thamani katika Wiki ya Umoja wa Kiislamu, na ninawaita ndugu wote kuwa na kiwango cha juu kabisa cha mshikamano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika vita vyake vya hatima dhidi ya majeshi ya kibeberu ya Marekani na Uzayuni.

Al-Khatib alisisitiza: Wito huu unatokana na ukweli kwamba umoja ni mmoja na nguvu ni moja, na jamii ya dunia ya Kiislamu pia ni kama mwili mmoja ambao kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine husimama pamoja nacho kwa kuumwa. Qur'ani Tukufu pia inasema:

«إِنَّ هَذِهِ أُمَّتُکُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّکُمْ فَاعْبُدُونِ».

“Kwa hakika Umma wenu huu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu, basi niabuduni.”

Alisisitiza: Huu ni ukweli ea Qur'ani ambapo matukio hayawezi kuibadilisha, bali yanaithibitisha; kama vile ambavyo namna ambavyo Magharibi inaulenga Ulimwengu wa Kiislamu na Waislamu pia wanathibitisha ukweli huu.

Mwisho, akizungumzia maneno ya Kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, alisema: Niruhusuni nihitimishe maneno yangu kwa nukuu hii yenye maana kubwa kutoka kwa Kiongozi Khamenei. Anasema: “Leo kuna nchi nyingi za Kiislamu na kuna takribani Waislamu bilioni mbili duniani, lakini mkusanyiko huu hauwezi kuitwa Umma; kwa sababu Umma unaundwa na watu wenye mlingano na wenye misukumo ya pamoja, ambao wanaelekea katika lengo moja. Lakini sisi Waislamu leo tumetawanyika.”

Aliongeza: Kama alivyosema Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, maadui wa Uislamu wamezitawala baadhi ya nchi za Kiislamu, na hisia ya baadhi ya nchi kuwa zinahitaji aina mbalimbali za uungaji mkono kutoka Marekani ni matokeo ya mgawanyiko wa Waislamu.

Kama Waislamu wasingekuwa wametawanyika, wangeweza kutumia uwezo na rasilimali za kila mmoja na kutegemea uwezo wao wenyewe, na kuunda mkusanyiko mmoja ulioungana ambao ungekuwa na nguvu zaidi kuliko madola yote makubwa, na ambao ungewaondolea ulazima wa kuitegemea Marekani.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha